MSAFARA WA MBUNGE KILWA KUSINI WAPATA AJALI.



Kilwa,
Mbunge wa jimbo la Kilwa kusini Mh. Selemani Bungara (Bwege) na msafara wake wamepata ajali katika eneo la Migelegele. 


Ajali hio imetokea wakiwa safarini kuelekea kjiji cha Likawage ikiwa ni moja ya ziara za Mh. Bungara za kutembelea vijiji ambavyo vipo ndani ya jimbo lake la kilwa kusini.


Kwa mujibu wa taarifa za awali zinasema kua hakuna aliepoteza maisha katika ajali hio ila kuna baadhi ya viongozi wamepata maumivu makali.


Chanzo kimesema Mkurugenzi wa siasa Bw. Deo Chaurembo amepata maumivu makali ya ndani kwa ndani na Katibu wa Mbunge Bw. Yusufu Saidi Abasi amepata maumivu kiasi huku Mh. Selemani Bungara akiwa salama kabisa.


Majeruhi hao wamefikishwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilwa (Kinyonga) kwa matibabu zaidi.

Bw. Yusufu Saidi Abasi akipata matibabu


Uongozi wa Mundunkolo.Blogspot unawapa pole ndugu zetu waliofikwa na ajali hiyo na mwenyezi mungu awasimamie waweze kupona haraka ili waendelee na majukumu ya kulijenga taifa.


Previous
Next Post »