KUNANI KILWA? NGISI MWENYE KILO ZAIDI YA 20 APATIKANA.



kilwa,

Kunani kilwa? Ndio swali ambalo unaweza  kujiuliza katika fikra yako baada ya kusikia maajabu yanayoendelea  kutokea   wilayani hapo.

Baada ya kuonekana samaki mkubwa miezi kadhaa iliyopita akiwa amekufa katika eneo la masoko pwani, wilaya ya kilwa hatimaye Ngisi mwenye ukubwa kuliko mazoea ameonekana    maeneo hayo ya masoko pwani.

Kwa mujibu wa chanzo chetu Ngisi huyo amekutwa anaelea akiwa amekufa ndipo akachukuliwa na kupelekwa nchi kavu kama ilivyo ada.

Baada ya kukaguliwa na wataalamu waligundua kua Ngisi huyo alikua amekufa siku za karibuni kwa kua alikua hajaanza kuharibika sana na baadhi ya mikia yake ilikua imekatwa kwa kuliwa na samaki baharini.

Baada ya kumpima alibainika kua na kilo 23 na gramu 700 hali ambayo ilistaajabisha watu wengi kwakua ni nadra sana kuona au kumpata Ngisi ambaye amezidi kilo 6 kwa sababu kwa kawaida Ngisi mwenye kilo nyingi hufikia kilo 5 hadi 6.

Diwani kata ya Masoko Mh. Abuu Mussa Mjaka akiwa amemshika Ngisi ambaye ana kilo 23 na gram 700.

Mundunkolo.Blogspot ilitaka kujua ni sababu zipi zilizopelekea Ngisi huyo kua na kilo nyingi kuliko mazoea? Swali ambalo lilijibiwa na Afisa uvuvi Wilaya ya Kilwa Bw. Mkali.

“Huyo Ngisi ni wa kawaida kama ngisi wengine ila amefikia hatua hiyo kwa kua alikua anakaa kwenye maji yenye kina kirefu, maji ambayo tofauti na yale ambayo wavuvi wanavuaga Ngisi wengine

Kwahiyo alikua anakaa sehemu ambazo ni mbali na maeneo ambayo wavuvi wa Ngisi wanafanya shughuli zao za kiuvuvi hali ambayo imepelekea kuishi kwa muda mrefu na kukua mpaka kufikia hatua hio” Alijibu

Amesema Ngisi huyo alisukumwa na mawimbi ya maji baada ya kua amekufa ndipo Mvuvi aliemuona akamchukua.

Aidha Bw. Mkali amewaambia wanainchi wasimtumie kwa chakula Ngisi huyo kwa kua bado haijajulikana sababu iliopelekea kufa kwa Ngisi huyo.

Kwa sasa Ngisi huyo anaonyeshwa kwa malipo ya Shilingi 500 kabla ya kufukiwa kwa kua hafai kwa matumizi ya kibinaadamu (Kuliwa).
 

Previous
Next Post »