Kilwa,
Mbunge wa jimbo la
Kilwa Kaskazini Mh. Vedasto Ngombale
ametembelea katika kijiji cha Kinywanyu
na kufanya mkutano na wananchi wa kijiji hiko.
Katika mkutano huo
uliohudhuriwa Na wananchi mbalimbali Mh. Ngombale aliwashukuru wananchi kwa
kumuanini na kumpa kura zilizotosha kumpa ushindi wa kiti cha ubunge katika
uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Aidha Mh. Ngombale
alikagua majengo ya Shule pamoja na kutoa vifaa vya michezo kwa vijana kijijni
hapo ikiwa ni jitihada za kuinua soka la wilaya ya Kilwa pamoja na ajira kwa
vijana.
Kinywanyu ni moja ya
vijiji ambavyo vinapatikana katika Jimbo la Kilwa Kaskazini ambalo linaongozwa
na Mh. Vedasto Ngombale baada ya kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
![]() |
| Mh. Vedasto Ngombale akiwa katika ziara yake kijijini kinywanyu. |
Sign up here with your email

ConversionConversion EmoticonEmoticon