Mabingwa watetezi wa
mshikamano cup, Black mob fc kutoka mji
kingunge wa Kilwa kivinje imekubali kipigo cha goli tatu kwa moja kutoka kwa
Mtibwa sugar wana tamu tamu katika mchezo wa kirafiki uliopigwa leo novemba
sita katika dimba la ukote mjini Kilwa kivinje.
Mchezo huo wa kukata na shoka umepigwa kwa dhumuni la
kutoa burudani kwa wepenzi wa soka wilayani Kilwa sambamba na kuonyesha vipaji
ambavyo vinapatikana Kilwa huku mtibwa sugar wakiutumia mchezo huo kama
kipimo kuelekea mchezo wao wa ligi kuu
dhidi ya ndugu zao wakata miwa Kagera sugar.
timu zote zilionekana
kuanza mtanange kwa kucheza mchezo wa kujihami
na kushambuliana kwa zamu kabla ya mkongwe Henry Joseph Shindika kukata
utepe wa magoli kwa kuiandika timu yake ya mtibwa sugar bao safi la kuongoza
katika dakika ya Thelathini na nane ya mchezo baada ya kuunganisha kwa kichwa
mpira wa kona uliopigwa kutoka magharibi ya uwanja.
Mpaka timu zinakwenda
mapumziko mtibwa sugar ilikua mbele kwa goli moja dhidi ya wapinzani wao.
Dakika kumi na nne mara
baada ya kuanza kwa kipindi cha pili mchezaji Kelvin Sabato akaifungia mtibwa
goli la pili katika mtanange huo na kufanya ubao usomeke goli mbili kwa mtibwa
na sifuri kwa wenyeji.
Kelvin sabato aliendelea
kuli didimiza jahazi la Black mob fc kwa kufunga goli la tatu kwa mtibwa sugar
na la pili kwake katika mtanange huo katika
dakika ya sitini na saba ya mchezo.
Zikiwa zimesalia dakika
kadhaa Black mob fc walifanya mabadiliko ya kiufundi na kuwaingiza wachezaji
wawili kwa pamoja, wachezaji ambao walisaidia kubadili mchezo na kufanikisha
kupata bao la kufutia machozi lililo wekwa wavuni na Anderson Rage katika
dakika ya Themanini na tatu ya mchezo kwa shuti kali lililo mshinda mlinda
lango wa mtibwa.
Black mob fc
walionekana kuchachamaa katika dakika za lala salama mara baada ya kuonja ladha
ya goli kwa kulisakama goli la mtibwa bila mafanikio.
Mpaka muamuzi Ahmadi
tiwa anapuliza kipyenga kuashiria kumalizika kwa pambano hilo mtibwa sugar tatu
black mob fc moja.
Baadaya mchezo huo
mundunkolo.blogspot ili bahatika kufanya mahojiano na golikipa namba moja wa
mtibwa sugar Benedict Tinoco alisema
“Tunashukuru mungu
mchezo umeisha salama na tumepata changamoto ya kutosha kuelekea mchezo wetu wa
ligi kuu dhidi ya kagera sugar katika uwanja wa nyumbani, na pia nawashauri
ndugu zangu wafuate miiko ya soka watafika mbali kwani vipaji wanavyo vya
kucheza timu yoyote inayoshiriki ligi kuu.
Akiwakilisha timu ya
black mob fc mchezaji Juma Jega amewashukuru waandaji wa mechi kuanzia ile ya
Lipuli, Ndanda na ya Mtibwa pia amewataka wachezaji amba bado hawajatoka kutumia
mechi hizo kama funzo kwao ili waweze kufikia malengo waliojiwekea kupitia
soka.
Mtibwa imesafiri
kuelekea morogoro ikiwa imecheza michezo mitatu ikiwa kusini mwa Tanzania
ukiwemo mchezo wa ligi dhidi ya Ndanda fc, na michezo miwili ya kirafiki.
picha zote na Ally Ruambo.
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon