Kilwa,
Mkurugenzi mtendaji wa
halmashauri ya wilaya ya Kilwa Bw. Zablon
Bugingo akiambatana na Baraza la madiwani na watalamu mbalimbali kutoka
Halmashauri ya wilaya ya Kilwa wamefanya ziara katika eneo linalotarajiwa kujengwa
kituo cha mabasi katika kjiji cha Nangurukuru.
Dhumuni la ziara hio
ikiwa ni kujiridhisha juu ya umiliki na uhalali wa wamiliki wa eneo hilo ambao
wanatarajiwa kulipwa fidia baada ya tathimini ili kupisha ujenzi wa kituo cha
mabasi katika eneo hilo.
Aidha Mkurugenzi
mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa Bw.
Bugingo wamewataka wananchi wote ambao wamehakikiwa katika uhakiki
uliofanyika kuwasilisha vielelezo vyao vyote ambavyo vinaonyesha uhalali wa
umiliki wa maeneo hayo katika ofisi ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya
wilaya ya Kilwa siku ya tarehe saba mwezi wa kumi na moja (07/11/2017) kwa
ajili ya kujiridhisha na kuendelea na hatua inayofuata.
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon