MHESHIMIWA NGUBIAGAI AWAONYA WANAO JICHUKULIA SHERIA MKONONI.



Mkuu wa wilaya ya Kilwa mhe. Cristopher Ngubiagai (katikati) na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kilwa Bw. Zablon Bugingo (wa kwanza kulia) wakimsikiliza moja ya wadai baada ya mkutano uliofanyika tarehe 19 mwezi huu  katika kijiji cha Lihimalyao.

Mkutano huo ulifanyika baada ya kupokea taarifa ya baadhi ya wakulima wa zao la korosho kufunga  ghala la kuhifadhia korosho kijijini hapo wakishinikiza kulipwa madai yao yaliyotokana na uuzwaji wa korosho zao msimu uliopita.

Akiambatana na kamati ya ulinzi na usalama mkuu wa wilaya aliwasihi wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani kwa kufanya hivyo wanakua wanaenda kinyume na sheria  za jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Aidha mkuu wa wilaya amewaomba wananchi ambao wanadai stahiki zao waendelee kua na subira kwani wanatambua kua wananchi hao wanadai na serikali iko macho kuhakikisha inawasaidia wakulima  hao kupata stahiki zao haraka iwezekanavyo.

Katika mkutano huo watu kadhaa walikamatwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kushiriki katika  mchakato wa kufunga ghala hilo na kuzuia wakulima wengine kuhifadhi korosho zao kwa ajili ya mauzo hali iliyopelekea kuhatarisha usalama wa mazao yao.

Previous
Next Post »