Kilwa,
Mkuu wa wilaya ya Kilwa Mh.
Christopher Ngubiagai amewataka wanainchi kutunza rasilimali ambazo mungu
amewajaalia kwa manufaa yao ya sasa na vizazi vijavyo.
Amesema endapo
rasilimali hizo zitatunzwa na kutengenezewa mikataba bora zitasaidia kusukuma gurudumu
la maendeleo kutoka lilipo sasa na kufikia uchumi wa kati.
Hayo ameyasema katika
hafla fupi ya makabidhiano ya jengo jipya la wodi ya kina mama ambao wanasubiria kujifungua (Mama Ngojea) katika Hospitali ya
wilaya ya Kilwa (Kinyonga) ambalo limejengwa kwa msaada wa Kampuni ya Uchimbaji
Gesi ya Pan African Energy yaliyofanyika katika viunga vya Hospitali hio mapema
wiki hii.
Pia Mh. Ngubiagai
amewaonya wavuvi ambao wanaendesha shughuli za uvuvi kwa kutumia zana ambazo
zimezuiliwa ikiwemo mabomu kuacha mara moja kwani zinahatarisha maisha ya viumbe
hai vinavyoishi baharini pamoja na mabomba ya gesi ambayo yapo chini ya bahari.
| Mkuu wa wilaya ya Kilwa Mh. Christopher Ngubiagai akizungumza na wananchi waliojitokeza katika Hafla ya makabidhiano ya Jengo la wodi ya kina mama Hospitali ya wilaya ya kilwa (Kinyoga). |
Aidha Mh. Ngubiagaiamemuagiza Mkurugenzi mtendaji kushirikiana na wataalamu kutoa elimu kwa
wananchi juu ya faida za kujiunga na mifuko ya bima za afya ambayo itawasaidia
kupata huduma za matibabu muda wowote, pia amemtaka kupata idadi ya wazee
katika wilaya ya Kilwa ili waweze kutengenezewa vitambulisho ambavyo
vitawaruhusu kupata huduma za afya bure.
Awali akizungumza
katika hafla hio Meneja uwajibikaji na huduma za kijamii Kampuni ya uchimbaji
Gesi Pan African Energy Nd. Andrew Kashangaki ameishukuru Halmashauri ya Wilaya
ya Kilwa kwa ushirikiano ambao inaendelea kuutoa kwa kampuni hio na kuahidi
kuendelea kushirikiana nao katika masuala mbalimbali ya kijamii.
Akihitimisha hafla hio
Mwenyekiti wa mji mdogo wa Kilwa Kivinje Bw.Mohamedi Peta amewashukuru Pan
African Energy kwa msaada wao na kuomba kuendelea na moyo huo wa kujitolea
Hospitalini hapo misaada mbalimbali ikiwemo vifaa tiba pamoja na Mashine ya
Mionzi ( X-ray Machine) kwani iliyopo Hospitalini hapo ina matatizo ambayo
yamepelekea kusimama kwa huduma za X-ray.
Jengo la Mama Ngojea limegharimu
kiasi cha shilingi Milioni mia moja themanini na sita (Mil.186) mpaka
kukamilika kwake na linauwezo wa kuchukua wakina mama zaidi ya 20 kwa wakati
mmoja hali ambayo itasaidia kupunguza mlundikano katika wodi za
wazazi hospitalini hapo pindi wanapo subiria kujifungua.
| Muonekano wa jengo jipya la Wodi ya wazazi(Mama Ngojea) lililo jengwa kwa msaada wa Kampuni ya Uchimbaji Gesi ya Pan African Energy katika Hospitali ya Wilaya ya Kilwa ( picha zote na Ally Ruambo) |
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon