kilwa,
Mabingwa watetezi wa
mashindano ya mshikamano cup Leceister city Fc kutoka yalipo makoa makuu ya
wilaya ya kilwa wamefanikiwa kutinga hatua ya fainali katika mashindano hayo yanayofanyika kila mwaka kuanzia mwezi wa
saba.
Leceister city
wamafanikiwa kusonga mbele baada ya kuiadhibu timu ya Arsenal fc kutoka kilwa
pande kwa goli 3 kwa 1 katika mchezo wa nusu fainali uliochezwa mapema
leo katika dimba la ukote.
Leceister city walikua
wakwanza kutikisa wavu wa timu pinzani baada ya mshambuliaji wao
machachali Mustafa Makacho jezi namba 9
mgongoni kuwaandikia bao safi la
kuongoza dakika ya 9 ya mchezo toka
kuanza kwa mtanange huo.
Rashid Mtengula aliiandikia Leceister City goli la pili dakika ya 21 ya mchezo baada ya
kuunganisha kwa shuti kali mpira ulikua
una ambaambaa baada ya kona iliyochongwa kutoka upande wa magharibi wa uwanja
na kufanya timu hiyo kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa magoli 2 kwa 0 dhidi ya
wapinzani wao.
 |
kikosi cha Leceister city fc wakipasha misuli moto kabla ya mtanange wao na Arsenal Fc (picha na Ally Ruambo)
Mbaruku mbaruku
akaifungia timu yake ya Arsenal bao la kufutia machozi dakika ya 53 kwa mkwaju
wa penati baada ya kufanyiwa madhambi
akiwa katika kumi na nane ya timu pinzani.
Mustafa makacho
akaendelea kua mwiba wa mashindano hayo bada ya kuzima matumaini ya mashabiki
na wachezaji wa Arsenl Fc kutoka Pande kwa Kutupia goli la 3 na la 2 kwake katika mchezo
huo baada ya kutumia vizuri makosa ya
mlinda mlango wa Arsenal Fc Machejo Machejo katika dakika ya 88 na kumfanya
afikishe magoli 8 katika mashindano
hayo.
Baada ya mtanange huo
kuisha mchezaji Yahaya Maliki kutoka Arseanal Fc alichaguliwa kua mchezaji bora
katika mpambao huo ulio isha kwa timu yao kufungwa goli 3 kwa 1.
 |
| Mchezaji wa Arsenal Fc Yahaya Maliki akipokea zawadi ya mchezaji bora wa mechi kati ya Arsenal na Leceister City. |
Kwa matokeo hayo
Leceister City itamenyana na Black Mob Fc (makuzi) katika hatua ya fainali ambayo
inatarajiwa kupigwa juma mosi ya kwanza ya mwezi wa 9 ( tarehe 02/09/2017) katika dimba la ukote.
Black Mob Fc imetinga
hatua ya nusu fainal baada ya kuitoa timu ya Kivinje Soccer Academy zote kutoka
mjini Kivinje kwa changamoto ya mikwaju ya penati 5 kwa 4 baada ya kutoka sare
ya kufungana goli 1 kwa 1 katika dakika 90 za mchezo.
Swali lililobaki
vichwani mwa wapenzi wa soka wilayani kilwa na viunga vyake ni nani atachukua
ubingwa wa mashindano ya mshikamano cup mwaka 2017? Je Leceister city watatea
ubingwa wao au Black Mob Fc ( makuzi) watachukua kwa mara ya pili baada ya
kuchukua ubingwa huo mwaka 2014?
| | | | | | | | | | |
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon