Zikiwa zimesalia siku
tisa kuelekea mchezo wa fainali mashindano ya Mshikamano Cup kati ya
Leceister City Fc dhidi ya Black Mob Fc (Makuzi) mbwembwe za viongozi na
mashabiki wa mpira wilayani Kilwa zimeanza kutawala.
Kila timu inajinasibu
kua itamaliza mchezo ndani ya dakika 90 kwa kuibamiza timu pinzani goli zisizo
pungua tatu na kuendelea.
Akizungumza na
mwandishi wetu Msemaji wa timu ya Black Mob Fc Bw. Shaweji Mamboya amesema timu yake ipo timamu kwa asilimia mia kuelekea
mchezo wa fainali licha ya kua na majeruhi mmoja ambaye anasumbuliwa na
matatizo ya nyonga lakini anaamini mpaka kufikia siku ya fainali atakua yuko
vizuri kwakua amekwisha anza mazoezi mepesi.
”Timu iko vizuri kwa
asilimia mia na tumejiandaa kukabiliana nao hao wapinzani wetu siku hiyo ya
fainali licha ya kua mchezaji wetu Mohamedi
Kituga kua na maumivu ya nyonga,
lakini nina imani mpaka kufikia siku ya mchezo atakua yuko vizuri kwa kua
amekwiasha anza mazoezi mepesi mepesi.
Niwatoe tu wasiwasi
wapenzi na mashabiki wa Black Mob Fc kua tutachukua ubingwa, Ng’ombe wawili na
zawadi zingine zitabaki kivinje.”Alisema
Bw. Mamboya amejinasibu
kua ana imani na safu yake ya ulinzi kwani mpaka kufikia hatua ya robo fainali
ilikua imeruhusu goli nne tu na kwa morali waliokua nayo wachezaji wake
hususani safu ya washambuliaji anaamini kabisa kua watamaliza mchezo huo ndani
ya dakika tisini kwa kumfunga Leceister city Fc goli 3 kwa nunge.
“Kwetu sisi mechi ya
nusu fainali ndio huwaga ngumu miaka
yote lakini hatujawahi kumuacha mtu salama katika hatua ya fainali.”
Alisisitiza Bw. Mamboya
Kwa sasa timu hio
inaendelea na kambi katika mji wa kilwa kivinje wakijiandaa kuwavaa mahasimu
wao Leceister City huku wachezaji wao mahiri Okwi na Manyanya wakionekana
kujifua zaidi ili kuimaliza Leceister City Fc katika mtanange huo wa fainali.
![]() | ||
| Wachezaji wa Black Mob Fc (Makuzi) wakiwa na nyuso za furaha baada ya ushindi. |
Kwa upande wao mabingwa
watetezi wa mashindano hayo Leicester City Fc wamesema wanataka kuudhihirishia
umma kua hawakubahatisha kuchukua ubingwa msimu uliopita kwa kuchukua tena
ubingwa msimu huu.
Wamesema wako vizuri na
mchezaji wao aliepata majeraha ameanza mazoezi mepesi na leo wanaanza rasmi
kambi kwa ajili ya maandalizi kuelekea katika mchezo wa fainali siku ya tarehe 2.
Mmoja wa waanzilishi wa
timu hiyo Bw. Hamisi almaarufu Udeze amesema hawana shaka kabisa juu ya ubingwa kwani ana
kikosi kizuri na safu bora ya washambuliaji ikiongozwa na mtu mwenye njaa ya
magoli Mustafa Makacho.
“Kuhusu ubingwa hilo
hatuna shaka nalo kabisa kwani nina kikosi imara ambacho kina uwezo wa kufanya chochote
katika mda wowote
Nadhani hata hao Black
Mob vichwa vitakua vinawauma sasa kwa kua wanajua kinachoenda kuwakuta kwani
hawana beki ya kumzuia Makacho na washambuliaji wengine, kwanza Makacho
anazijua beki zao zote na udhaifu wao kwahiyo hawatamsumbua.” Alijinadi Udeze
Homa ya mashabiki na
wapenzi wa mpira wa miguu wilayani kilwa na viunga vyake imezidi kupanda
kuelekea katika mchezo wa fainali unataraijwa kupigwa juma mosi ya kwanza ya
mwezi wa tisa kwa kuzikutanisha timu zenye majina makubwa katika soka la wilaya
ya Kilwa Leceister city toka kilwa Masoko na Black Mob Fc au Makuzi kama wengi
wanavyopenda kuuita kutoka Kilwa Kivinje.
Ni mchezo ambao utakua
wa kukata na Shoka kwa kua unakutanisha timu kutoka miji miwili tofauti iliyo
karibu ambapo mmoja anataka heshima kwa kubakiza ubingwa nyumbani na mwengine
anataka heshima ya kupeleka ubingwa nyumbani kwa mara aya pili mfululizo.
Nani kuibuka na kicheko
na nani kuibuka na kilio? Jibu litapatikana siku ya tarehe 2 katika Dimba la
ukote mjini Kilwa Kivinje kuanzia majira ya saa kumi jioni ambapo
Mundunkolo.Blogspot itakua inakuletea moja kwa moja kitakacho kua kinajili katika mtanange huo.
Sign up here with your email

ConversionConversion EmoticonEmoticon