MBARONI KWA TUHUMA ZA KUJIUSISHA NA UVUVI KINYUME NA SHERIA.



             

Kilwa, 

       Jeshi la polisi wilaya ya kilwa linawashikilia watu zaidi ya 30 kwa tuhuma za kujihusisha na shughuli za uvuvi kinyume na sheria.

Wavuvi hao wamekamatwa Jana katika operesheni maalum ambayo iliongozwa na Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya kilwa Mh. Christopher Ngubiagai katika kambi ya wavuvi hao inayojulikana kwa jina la Msangamla, Kilwa Kisiwani.

Operesheni hio imekuja baada ya kupokea malalmiko kutoka kwa wanainchi juu ya ukiukwaji wa sheria uliokua unaendelea katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na uvuvi usiofuata sheria, matumizi ya madawa ya kulevya aina ya bhangi.

Akizungumza na mwandishi wetu Afisa uvuvi wilaya ya kilwa Bw.Hussein Rambo amesema wameamua kufanya oparesheni hio ikiwa ni njia moja wapo ya kuthibiti Wavuvi wahamiaji ambao wanavua bila yakua na vibali kutoka mamlaka husika pamoja na kupunguza wimbi la vitendo vya uvuvi haramu.

Amesema kwa yeyote anayetaka kuendesha shughuli za uvuvi wilayani kilwa anakaribishwa, lakini afuate sheria na kanuni kama baadhi ya wavuvi kutoka sehemu mbalimbali nje ya kilwa walivyofanya.

“Tunamkaribisha mtu yeyote kuja kufanya shughuli za uvuvi wilayani kilwa ila afuate sheria ambazo zimewekwa “alisema

Bw. Rambo amesema ili uweze kutambulika na kufanya shughuli za uvuvi wa kuweka makazi (Dago) wilayani kilwa na viunga vyake inabidi ufuate misingi ya sheria kwa kufanya mambo kadhaa ikiwemo:-

Mosi, mvuvi inabidi awe na barua ya utambulisho kutoka kwa Afisa uvuvi ambako mvuvi anatoka ikiwa imeambatanisha na Leseni ya Uvuvi.

Pili, Muombaji atawasilisha vielelezo hivyo , na baadae atakutana na Bmu ya sehemu husika ambapo watamjadili pamoja na kukagua zana zake za kazi kama zinaendana na sheria na kanuni za uvuvi, baada ya Bmu kuridhia Mwombaji ataonana na Afisa Uvuvi wa wilaya na kupatiwa Kibali cha kuendesha shughuli za uvuvi ambacho kitadumu kwa muda wa miezi mitatu.

Baada ya miezi mitatu kupita Mvuvi ataenda kwa Afisa uvuvi kwa ajili ya kupewa tena Kibali kama atahitaji kuendelea na shughuli za uvuvi.
 
watuhumiwa wakiingia katika gari

Akikanusha shutuma juu ya tukio hilo Bw. Rambo amesema sio kweli kwamba wakazi wa Kilwa Kisiwani hawataki Wavuvi wahamiaji bali ni utaratibu ambao upo na unatumika si Kilwa Kisiwani tu bali hata sehemu zingine.

“Sio kweli kwamba wakazi wa Kilwa Kisiwani hawataki wavuvi kutoka nje ya kitongoji chao bali ni utaratibu ambao upo kwamba , inabidi uwe na vibali ambavyo vinakutambulisha kua wewe ni nani na umetekea wapi  kwa sababu za kiusalama zaidi”. aliongeza

Aidha Bw. Rambo amewashauri wanainchi wa Kilwa na kutoka nje ya Kilwa kufuata sheria ili kuepukana na mkono wa sheria.

Katika operesheni hio ilioendeshwa na kamati ya ulinzi na usalama , maafisa uvuvi, Bmu pamoja na baadhi ya viongozi kutoka katika kitongoji hiko nyavu za kioo (monofilament net) pamoja na Mabanda kadhaa ambayo yalikua yanatumiwa na wavuvi hao yameteketezwa kwa  moto .
First