Kilwa,
Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya
Wilaya ya Kilwa Nd. Zablon Bugingo amekabidhi miradi ya barabara Kwa Meneja wa
TARURA Wilaya ya Kilwa Mhandisi Respicius Matungwa.
Makabadhiano hayo
yamefanyika mapema leo tarehe 31.08.2017 katika ofisi ya mkurugenzi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa mbele ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya
kilwa Mh. Abuu Mussa Mjaka, Mwanasheria wa Halmashauri Bw. Yusuf Msosa na
aliyekua Mhandisi wa Halmashauri Nd.
Chande.
Hatua hio imefikiwa ikiwa
Ni utekelezaji wa agizo la serikali la kubadili usimamizi wa miradi ya Barabara
kutoka katika Mamlaka za serikali za mitaa kwenda kwa Wakala wa Barabara za
Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA).
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndugu.Zablon I.Bugingo (Katikati) akimkabidhi miradi ya Barabara Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilwa Eng.Respicius C. Matungwa kutoka kulia ni Mwanasheria wa Halmashauri ya Kilwa Ndugu Yusufu Msosa, Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Abuu Mussa Mjaka.
Akitoa shukrani zake za
dhati baada ya kukamilika wa makabidhiano hayo Mkurugenzi wa Halmashauri ya
wilaya ya Kilwa Nd. Zablon Bugingo amesema anashukuru sana kwa kufanikisha
makabidhiano hayo na kuahidi kutoa ushirikiano wa hali na mali kwa Wakala huyo
.
TARURA( Tanzania Rural
and Urban Agency) ni wakala wa Barabara wa za vijijini na mijini Tanzania
ambaye ameanzishwa rasmi kwa dhumuni la
kusimamia shughuli zote zinazohusiana na Barabara ambazo awali zilikua
zikifanywa na Mamlaka za serikali za mitaa.
Sign up here with your email
2 comments
Write commentsUpo vizuri kiuandishi waitendea haki kalamu yako mungu Akuongoze
ReplyAsante sana
ReplyConversionConversion EmoticonEmoticon