BASI LATEKETEA KWA MOTO NANGURUKURU.



Kilwa,

Basi mali ya kampuni ya Ibra Express inayofanya safari zake kati ya Dar es salaam na Masasi limeteketea kwa moto.

Mkasa huo umetokea jana maeneo ya Nangurukuru Wilayani Kilwa takribani kilomita 2 kutoka Nangurukuru mjini.

 Basi hilo lilikuwa linatokea jijini Dar es salaam kuelekea Mjini Masasi.

Basi - Ibra Express likiwa linawaka moto

Taarifa za awali kutoka katika chanzo chetu zinasema hakuna aliyepoteza maisha wala kupata majeraha katika mkasa huo.

Mpaka habari hii inatoka chanzo cha moto uliopelekea kuteketea kwa Basi hilo bado kilikua hakijafahamika, huku mashuhuda wakidai wenda hitilafu katika mfumo wa umeme katika basi hio ndio umepelekea gari hio kuteketea kwa moto.

 

Previous
Next Post »