Kilwa,
Timu ya Kichanga chui
Fc imefanikiwa kusonga mbele katika mashindano ya ligi daraja la nne ngazi ya
wilaya, wilaya ya Kilwa.
Kichanga chui imesonga
mbele baada ya kuitupia nje ya mashindano timu ya Al qaeda Fc kutoka
Kilwa masoko kwa kuichapa goli moja kwa sifuri katika mchezo uliopigwa jana
katika uwanja wa Mwenge (Taifa) mjini Kilwa masoko.
Katika mtannage huo wa kukata na shoka timu zote zilionyesha kucheza mchezo wa kushambuliana na kujihami sana hali iliyopelekea kutopatikana
kwa mbabe mpaka muamuzi anapuliza kipyenga kuashiria mapumziko.
Kipindi cha pili milango ya timu zote iliendelea kuwa migumu licha ya mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kwa
washambuliaji wa timu zote mbili kabla ya Dickson Ngenje kuiandikia timu yake
goli pekee katika dakika za lala salama za mtanage huo.
Kwa matokeo hayo timu
ya Al qaeda Fc inaaga mashindano hayo na kuungana na timu za Mihina Fc, Ngome
Fc , Tamofa Fc na zinginezo ambazo zimeipa mkono wa buriani timu ambazo zinaendelea
na mashindano hayo yanayotarajiwa kufikia tamati wiki hii.
Timu ya Al qaeda imeyaaga mashindano hayo baada ya kutoka suluhu dhidi ya Mihina Fc, sare ya goli moja kwa moja dhidi ya kichanga chui Fc, kipigo cha goli 3 kwa 2 dhidi ya Kilwa youth soccer academy, kabla ya kukubali kipigo cha goli 1 nunge dhidi ya Kichanga chui Fc.
Jumammosi ya wiki hii Kichanga
chui Fc itakua uwanjani wakimenyana na Kilwa youth soccer academy ili kumpata
bingwa wa kituo cha masoko (Kilwa Kusini) ambaye ataungana na bingwa wa Kilwa
kaskazini katika kuiwakilisha wilaya katika ngazi ya Mkoa (ligi daraja la
tatu).
Bingwa wa Kilwa
Kaskazini atapatikana katika mtange ambao utawakutanisha Al qaeda Fc kutoka
Njianne ambaye ni bingwa wa kituo cha Njianne dhidi ya bingwa kutoka kituo cha somanga Casablanca Fc katika mchezo unaotarajiwa kupigwa siku ya ijumaa
katika dimba la ukote mjini Kilwa Kivinje.
Akizungumza na Mundunkolo.Bolgspot.com Naibu
katibu mkuu, Chama cha Soka Wilaya ya Kilwa (KILFA) Nd. Ally Liyoka amesema
anashukuru mashindano yanaendelea vizuri licha ya kukumbwa na changamoto za
hapa na pale hususani swala la ukata kwa vilabu ambavyo vinashiriki ligi hio.
Amesema timu nyingi
zimeshindwa kufanya usajili mzuri na maandalizi ya kutosha kwa kua hazina uwezo
wa kifedha wa kugharamia gharama hizo hali ambayo imepelekea timu nyingi
kushindwa kujitokeza na zilizo jitokeza kushindwa kumudu baadhi ya gharama.
“ukiachana na ukata wa
timu lakini pia tunachangamoto katika swala la waamuzi lakini sisi kama
viongozi tunajitahidi kulitafutia ufumbuzi.” alisema Bw.Liyoka
Sign up here with your email
ConversionConversion EmoticonEmoticon