SEVILLA FC YANYUKWA 2-0 PAMBANO LAVUNJIKA.



Kilwa,

        Timu ya sevilla fc   kutoka kilwa masoko imekubali kipigo cha goli mbili kwa nunge kutoka kwa ndugu zao wa Kilwa Youth Soccer Academy kabla ya mpambano huo kukatishwa kwa vurugu.

 Wachezaji wa kilwa youth soccer academy wakiwa mbele kwa goli 2 kwa bila wali amrishwa kutoka nje ya uwanja baada ya mchezaji mwenzao kuchezewa madhambi.

Samuel Galafao mwalimu wa Kilwa Youth Soccer Academy alikiamuru kikosi chake kitoke uwanjani kwa kile alichodai kuwa walikua wanachezewa michezo isiyokua ya kiungwana hali ambayo ilikua iki hatarisha afya ya wachezaji wake licha ya kutoa onyo mara kadhaa.

Mchezo huo  wa kirafiki umepigwa mapema leo katika uwanja wa Mwenge (Taifa) mjini kilwa masoko ikiwa ni mchezo wa  kujipima nguvu kwa timu hizo pamoja na  kusindikiza sherehe za sikukuu ya  iddi elhaji ambayo imesherehekewa leo duniani kote.
kiranja wa Sevilla Fc Selemen Charahani (Kushoto) akichuana na Juma Mbaga katika mechi ya kirafiki ilioisha kwa Kilwa Youth Soccer Academy kuibuka na ushindi wa goli 2 kwa 0 (picha na Ally Ruambo)

Mohamedi Hafidhi ndie aliye anza kutikisa wavu wa sevilla Fc baada ya pasi za hapa na pale, goli ambalo lilidumu mpaka mwamuzi alipopuliza kipyenga cha mapumziko.

Kipindi cha pili kilionyesha mabadiliko  kwa timu hizo  kushambuliana  kwa  zamu kabla ya Juma Mandai (Kaseja)  kuitimisha kalamu ya magoli kwa kuipachikia timu yake  Kilwa Youth Soccer Academy goli ambalo lilidumu mpaka pale mpambano huo ulipokatishwa kutokana na vurugu zilizo jitokeza.

Baada ya mtanange huo kuvunjika wadau mbali mbali wa soka walimtaka Kiongozi wa Sevilla Fc kuongea na wachezaji wake juu ya swala zima la nidhamu pamoja na kucheza michezo ya kiungwana kwani  mchezo wa soka ni wa  amani na sio uadui.

Kwa upande wake kiongozi wa Sevilla Fc alikubali na kuomba  msamaha kwa niaba ya timu yake  na kuahidi kua matukio kama hayo  hayatojitokeza  tena.

 

Previous
Next Post »